JAMII imetakiwa kujenga mahusiano na kujiepusha na ukatili wa kijinsia unaosababisha kuvunjika hovyo kwa ndoa na kuchangia kuongezeka kwa kundi kubwa la watoto wa mitaani na wanaojihusisha na biashara za ukahaba Kauli hiyo imetolewa katika kikao kazi kinachotathmini utekelezaji wa mradi wa jinsia unaohamasisha usawa wa kijinsia na fursa sawa za kiuchumi kwa wanawake na vijana unaendeshwa mkoani Lindi na asasi isiyo ya kiserikali ya LIWOPAC.
Katika kikao kazi hicho ambacho kilifanya tathmini ya utendaji wa mradi huo wa robo mwaka kuanzia Julai hadi Septemba, Ofisa Mradi wa LIWOPAC, Mwendo Mnambala pamoja na Afisa Ustawi wa jamii manispaa ya Lindi walizitaka jamii kuacha kudumaza haki na usawa wa kijinsia na kustawisha ukatili wa kijinsia. KARIBU COM TV , Television ya Mtandaoni ambayo imejidhatiti katika kuakikisha unapata habari ,Matukio ,Burudani za ndani na nje ya Tanzania kwa uharaka na uwakika.
Unaweza kutupata kwenye mitandao ya kijamii kama hivi INSTAGRAM : https://www.instagram.com/p/CPIn1ZNhB...