Siku ya Mtoto wa Kike Duniani
Siku ya Mtoto wa Kike Duniani
Tarehe 11 ya mwezi wa 10 kila mwaka ni siku ya maadhimisho ya mtoto wa kike duniani. Halmashauri ya Manispaa ya Lindi imeadhimisha siku hii muhimu katika uwanja wa mpira wa Ilulu ambapo hafla ya maadhimisho hayo yamehudhuriwa na watu na taasisi mbalimbali.
Miongoni mwa taasisi hizo ni pamoja na EWAGITA, KIWOHEDE, TAWCO, Restless, LIWOPAC, LISAWE, ROWODO, Dawati la jinsia mkoa na wilaya na Mtandao wa kijinsia Tanzani. Mgeni rasmi wa maadhimisho hayo ni Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya jamii Ndugu Moses Mkoveke akimuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Lindi Ndugu Shaibu Ndemanga.
Manispaa ya Lindi imeungana na Halmashauri zingine ambapo inatekeleza maadhimio ya Baraza kuu la Umoja wa Mataifa ambalo liliadhimia kuanzisha maadhimisho haya tangu mwaka 2011. Kuli mbiu yam waka huu ni “Haki zetu ni Hatima yetu,Wakati ni sasa”.
Maadhimisho hayo yamehusisha mambo mbalimbali ikiwemo maigizo na ngonjera zenye kupinga ukatili wa kijinsia na ajira za watoto kwani miaka ya sasa matukio ya ukatili wa kijinsia ni mengi hivyo kupitia maadhimisho haya watoto wamefundishwa jinsi kupinga lakini pia wakifanyiwa ukatili ni wapi wanapaswa kutoa taarifa.
Aidha, Mgeni rasmi Bwana Mkoveke amesema“Jukumu letu ni kuhakikisha haki na usawa katika jamii zetu inapewa kipaumbele.Hivyo natoa wito kwa jamii nzima ya wananchi wa Halmashauri ya LINDI kuunga mkono juhudi za serikali na wadau kusaidia upatikanaji wa haki za watoto wa kike, kupinga vikali mila potofu ili kuendelea kudumisha taifa linalojali amani na misingi ya haki za binadamu na hivyo kuboresha na kuinua usawa katika jamii zetu”.
Event details
-
Date
11-Oct, 2022 08:00 AM
11-Oct, 2022 04:00 PM -
Duration
8 Hrs -
Organizer
LIWOPAC -
Email
info@liwopac.or.tz -
Location
Uwanja wa mpira wa Ilulu, manispaa ya Lindi